Saturday, September 15, 2012

JUKWAA LA VYUO: KIJUE CHUO KIKUU CHA TAIFA ZANZIBAR (SUZA), CHUO KILICHOPO KANDO KANDO MWA FUKWE ZA BAHARI YA HINDI, VISIWA VYA UNGUJA



Leo katika makala yako ya historia za vyuo vikuu tunakuletea historia fupi ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (The state University of Zanzibar) kwa kifupi kinajulikana kama SUZA. Chuo ambacho ikinapatikana katika mwambao wa Bahari ya Hindi katika mji mkongwe wa Stone Town huko visiwani Zanzibar.

SUZA kilianzishwa mwaka 1999 ambapo mwaka mia miwili baadae yaani 2001 ndipo kilianza rasmi shughuli zake za kitaaluma. Katika jitahada zake za kutoa elimu bora, SUZA kwa muda mfupi kimeweza kufikisha lengo la kutoa elimu bora katika kanda ya nchi za Afrika. Kama chuo kikuu cha umma, SUZA inalenga kutoa elimu husika kwa walengwa katika kuharakisha mabadiliko ya kijamii na mabadiliko chanya ya kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kisiasa.
Dr. Ali Mohammed Shein
Mkuu wa Chuo (SUZA)
Chuo hiki kimeanzishwa chini ya kifungu Na. 18 sheria ya mwaka 1999 ya baraza la wawakilishi Zanzibar. SUZA kimenzishwa ili kuendesha kozi zitakazo zalisha walimu wenye utaalamu ambao watafundisha katika shule za sekondari pamoja na kulinda, kuwezesha, na kusambaza elimu katika masomo ya sanaa, sayansi na teknolojia.
Ikiwa ni miaka kumi sasa toka kuanzishwa kwake, SUZA kimejitanua zaidi kwani kina matawi mawili na kipo mbioni kufungua tawi la tatu yote yakiwa katika visiwa vya unguja. Tawi kongwe kabisa ni lile la Beit-el-Rasi, tawi liliotakana na chuo cha kwanza cha uwalimu Afrika Mashariki. Tawi hili lipo pembezoni mwa fukwe za Bahari ya Hindi, umbali wa kilomita tano kutoka mji mkongwe wa Stone Town.

Tawi lengine ni tawi la Vuga, lilipo kati kati ya mji wa Stone Town, ni majengo ya kihistoria yanayotumiwa na Chuo hiki katika tawi la Vuga na kukifanya kivutie kwa mazingira yake. Tawi la Vuga limezungukwa na na huduma za kijamii pamoja na ofisi za umma.
Dr. Ahmad Hamada Khatibu
Makamu Makamu Mkuu wa Chuo
Mipango, Utwala na Fedha
(SUZA)
 
Prof. Idris A. Rai
Makamu Mkuu wa Chuo
(SUZA)
 
Hivi karibuni SUZA inatarajia kuongeza Tawi lengine katika shabaha ya kuongeza wigo wa kutoa elimu bora, Tawi la Tunguu ni tawi la tatu na jipya litakalofunguliwa hivi karibuni. Tawi hili lipo umbali wa Kilomita 12 kutoka mji wa Stone Town. Mandhari yake ya kijani, tawi hili linalifanya liwe na miundombinu bora na ya kuvutia yenye kiwango cha kimataifa. Mipango ya chuo ni kuongeza matawi mengi zaidi ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo.
SUZA ni moja kati ya chuo kinachoongoza katika Visiwa vya Zanzibar, hii inatokana na ukuaji wa haraka wa chuo hiki ambapo kila mwaka kuna ongwezeko la wanafunzi wanaojiunga na chuo hiki. Kwa chuo kidogo kilichoimarika hivi karibuni, sasa chuo kina wanafunzi 1,205 na kati ya hao wanafunzi 693 wanasoma shahada ya kwanza katika fani mbalimbali.
Mrs. Ramla Mohammed
Mlezi wa wanafunzi
 
Kwa sasa Chuo kina Taasisi ya Kiswahili na Lugha za kigeni ambapo raia kutoka ndani na nje ya nchi wanapata kujifunza lugha mbalimbali duniani, Shule ya Uwalimu, Sanaa na Sayansi (SEAS), Taasisi ya Elimu ya kujiendeleza (Institute of Continuing Education), na Chuo cha Kompyuta. Chuo kinatarajia kufungua shule mbalimbali huko baadae katika njia ya kujpanua zaidi.




Majengo mapya ya SUZA yanaomaliziwa kujengwa ya katika Tawi la Tunguu, visiwani Unguja
Katika kuhakikisha kwamba kinajitanua zaidi, SUZA inaendelea kujenga majengo bora yenye muonekanao wa kihistoria, hili ni jengo la utawala lilopo katika kampasi mpya ya Tunguu nje kidogo mwa mji wa kihistoria wa Stone Town.

No comments:

Post a Comment